Kitaifa

Gazeti makini

Philipo Mulugo

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Sunday, November 10, 2013

Zitto: Nimechoka Kuzushiwa na kuchafuliwa

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe Na Agatha Charles, TaboraNAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ameibuka na kutoa kauli na tamko dhidi ya tuhuma mpya dhidi yake zilizosambazwa katika mitandao ya intaneti katika siku za hivi karibuni.Zitto, ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Kigoma Mjini, amefanya hivyo akitumia majukwaa mawili tofauti.Mwanasiasa huyo kijana...

Kenya yamuunga mkono JK

Rais Jakaya Kikwete Na Benjamin Masese, Dar es SalaamWAZIRI wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed, ameipongeza Tanzania kwa hatua ya kutangaza kuwa haiko tayari kutoka katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kama ilivyodhaniwa hapo awali.Akizungumza Dar es Salaam jana, alisema Kenya inaunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa Novemba 7, mwaka huu kuwa haitajitoa na wala haitakuwa chanzo cha kuvunjika kwa EAC.Alisema bila Tanzania...

Lowassa: Nasikitishwa elimu duni shule za kata

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa WAZIRI Mkuu mstaafu na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, amesikitishwa na kiwango duni cha elimu katika shule za sekondari za kata na baadhi ya vyuo vya elimu ya juu. Akizungumza katika harambee ya kuchangia mfuko wa elimu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama, alisema kiwango cha elimu katika shule hizo kinamsikitisha kwa kuwa ni...

Tuesday, November 5, 2013

Taswira ya Tanzania kiuwekezaji yadorora

Taswira ya Tanzania kiuwekezaji yadorora *Rushwa, miundombinu, umeme vyaiponza*Yashika nafasi ya 145 kati ya mataifa 189*Nyota ya Rwanda yang’ara kimataifa Na Gabriel Mushi TASWIRA ya Tanzania katika ubora wa mazingira ya kiuwekezaji na kwa kuwa na fursa zinazovutia biashara kimataifa imeendelea kuporomoka, Rai Jumatano limebaini. Ripoti mbili za kimataifa zilizotolewa na taasisi mbili za kiuchumi na kibiashara zinazoheshimika, Benki ya Dunia...

Elimu ya Tanzania imekosa mkombozi

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo NA ELIZABETH HOMBO NIMEKUWA nikitatizwa na mfumo wa elimu nchini, ingawa nami ni mmoja wa watu waliopitia kwenye mfumo huo, lakini ukweli ni kwamba umekuwa hauna tija kwa wananchi. Mfumo wa elimu na sekta ya elimu kwa ujumla imetawaliwa na matatizo. Waathirika wakubwa kwenye suala hilo ni Mtanzania fukara mwenye kipato kisichoeleweka. Kukosa kwake uwezo wa kumsomesha mtoto wake kwenye...

Kujiuzulu ni uadilifu wa kukiri upungufu

MTU anapokubali nafasi ya uongozi, maana yake ni kwamba anakubali kubeba wajibu mzima kuhusiana na ufanisi wa majukumu yake mahali pale anapopaongoza.Kwa bahati mbaya sana, viongozi wetu nchini ni wepesi wa kupokea sifa kutokana na utendaji mzuri wa wale walio chini yao. Lakini mambo yanapokwenda vibaya, viongozi hao hao ndio huwa wa kwanza kujiweka mbali na makosa yaliyotendeka.Tunasema kuwa kimsingi “kujiuzulu” si sawa na “kukiri kosa” moja kwa moja kwamba umelitenda. Kinyume chake, kujiuzulu ni tabia ya uadilifu, ambapo mhusika anakiri...

Wednesday, October 30, 2013

Mbowe ataka wahamiaji haramu walipwe fidia

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe Na Debora Sanja, Dodoma: KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (Chadema), ametaka wahamiaji haramu walioondoshwa nchini kwa kufanyiwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu walipwe fidia. Akiuliza swali la nyongeza bungeni jana, Mbowe alisema zoezi la Operesheni Kimbunga halikuwa na maandalizi ya kutosha na lilifanyika kwa chuki na uonevu. “Waliokuwa wanafanya zoezi hili hawakujali mali...