Kitaifa

Gazeti makini

Wednesday, October 30, 2013

Mbowe ataka wahamiaji haramu walipwe fidia

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Na Debora Sanja, Dodoma:
KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (Chadema), ametaka wahamiaji haramu walioondoshwa nchini kwa kufanyiwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu walipwe fidia.

Akiuliza swali la nyongeza bungeni jana, Mbowe alisema zoezi la Operesheni Kimbunga halikuwa na maandalizi ya kutosha na lilifanyika kwa chuki na uonevu.

“Waliokuwa wanafanya zoezi hili hawakujali mali za wananchi, hawakuangalia mazingira yaliyosababisha mtu kuwepo nchini na uchunguzi wa kutosha haukufanyika,” alisema.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha alisema zoezi hilo la kuwaondoa wahamiaji haramu lilikuwa na nia njema.

Alisema ni kweli yapo malalamiko ya jinsi zoezi hilo lilivyokuwa linatekelezwa na kwamba Serikali itafanya kila linalowezekana kulichunguza jambo hilo.

Alisema ikibainika utaratibu wa kuwaondoa wahamiaji hao ulikiukwa, sheria zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria.

0 comments:

Post a Comment